Friday, November 27, 2009

NICE WEEKEND

JAMANI WEEKEND NJEMA NA SIKUKUU NJEMA YA IDD-EL-HADJ
JJUMAPILI MIE NITAKUWA UWANJA WA SOKOINE KUFIESTIKA. KAMA VIPI J3

Thursday, November 26, 2009

BAADHI YA WAFANYAKAZI WA MBEYA FM

JACKLINE CHARLES
BURHAN SAID dj Acrama
ERICK KAZONDA

ABDULMAJEED MOHAMED.studio manager
ERNEST MBWILE dj Nest
AMIRY ABDALAH. smart B

TULIANZA KAMA TIMU

Hii picha haionekani vizuri naomba mniwie radhi lakini hawa ni baadhi tu ya watangazaji wa mbeya fm wengine hawapo pichani, lakini wanne kati yao hatupo nao tena kutokana na sababu zao lakini wawili ni kutokana na utovu wa nidhamu na hao 2 waliamua, kama tunavyojua akiondoka mtu anaingia mtu baada ya siku 3 tukapata watu wengine watano. napenda sana rangi ya pinki.

HAWA WAKAJIONDOA KWENYE TIMU

Huyu anaitwa Peter Mlangi a.k.a dj P, alikuwa dj wetu lakini akaona kukaa mbali na my wife wake ni noma akaamua kuondoka na kwenda DSM kwa my wife wake. Alikuwa na busara sana na ni muelewa sana ila jamaa ana hasira ukimuudhi tu yeye ana mkono mwepesi sana, kwa hiyo haoni noma kukupa chako, nakukumbuka sana my brother
Anaitwa Ambwene Christopher alikuwa ofice administrator wetu na alikuwa my best friend lakini kaamua kuondoka, nitakukumbuka daima my friend.

Wednesday, November 25, 2009

Sunday, November 22, 2009

HIVI NDIVYO MBEYA FM ILIVYOFANIKISHA MICHUANO YA KAPUNGA CUP 21.NOVEMBER.2009


"oooooyyyeeeeeeee"yaaani hadi raha jamani. haya kijana kamata mkwanja wako huoo.
washindi wakiwa katika picha ya pamoja huku wakiwa wameshika kombe lao.



MBEYA FM imeweza kufanikisha michuano ya Kapunga Cup ambayo ilianza rasmi tarehe
28.10.2009. michuano hii ilishirikisha timu za kata 36 za jiji la mbeya, na ziliundwa kanda nane
ambazo zilicheza hatua ya kwanza ambazo ndizo zilizokuja kucheza hatua ya robo fainali hadi fainali.

Fainali zimefanyika jana 21.11.2009 katika uwanja wa Ruanda Nzovwe na ilishirikisha kanda E na C.Kama tunavyojua katika mashindano lazima mshindi apatikane,

Kanda E iliibuka kidedea kwa penati na kuweza kujinyakulia kitita cha shilingi laki 5 kombe pamoja na jezi seti moja,
Mshindi wa pili alijinyakulia kitita cha shilingi laki 3, kombe dogo na jezi seti moja,
Mshindi wa tatu aliibuka na kitita cha shilingi laki moja na jezi seti moja.mfungaji bora alijinyakulia kitita cha shilingi elfu hamsini na ngao ya mfungaji bora.

Dhumuni la michuano hii ni kuhakikisha vijana wanapata nafasi ya kubadilishana mawazo, kuwaepusha na matumizi ya dawa za kulevya na makundi yasiyokuwa na msingi ambayo mwisho wake ni uhalifu. vilevile kupitia michuano hiyo tumefanikiwa kupata wachezaji watatu watakaojiunga na timu ya Tanzania Prisons inayoshiriki ligi kuu katika kipindi cha dirisha dogo la usajili wa ligi kuu ya soka Tanzania.

Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya ATHANAS KAPUNGA ameishukuru MBEYA FM RADIO kwa kuandaa na kudhamini michuano hiyo kwa mwaka 2009.
MICHEZO FURAHA........... MICHEZO AFYA.................... MICHEZO HUJENGA MAHUSIANO MEMA.

HAYA KIJANA NA WEWE SHIKA HIZI

mmoja wa wachezaji wa kanda C ambao walikuwa washindi wa pili akipokea zawadi ya kombe dogo, seti moja ya jezi na kitita cha shilingi laki tatu

MDAU WA SOKA KATIKA SHANGWE


mdau wa soka toka pande za Kanda E akiwa ni mwenye furaha na akishangilia ushindi wa timu yake ambayo ndio iliyoibuka kidedea siku hiyo baada ya kushinda kwa mikwaju ya penati.ushindi raha jamani

MEZA KUU

meza kuu ikiwa imesheheni zawadi

MAUZO YA UKWELI

mtoto wa mzee nanihii mwenyewe nikiwa katika pozz
wadau wa Mbeya Fm tukijiachia kwa raha zetu,mara tu baada ya mpira kumalizika.
washindili wa ligi za Kanda,wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Mbeya Fm ambao ndio waliokuwa wadhamini wakuu wa mashindano hayo.
mauzo muhimu japo kwa siku moja moja.

KAKA KAZI ZA WATU HIZOOO

sijui huyu amejifunzia wapi kufanya alichokuwa anafanya, aliambiwa alinde yeye akaamua kuchabo, anaitwa ABDULMAJEED MOHAMED, manager wa 89.5 MBEYA FM

KABLA YA MECHI

refarii akiwa na malaizmen wake pamoja na makapteni wa timu zote mbili.
kikosi cha timu ya Kanda C katika picha ya pamoja(sijui huyo kepteni wa timu pinzani kafata nini huku?)
kikosi cha timu ya Kanda E katika picha ya pamoja.
Manager naye hakuwa nyuma katika ukaguzi wa timu.
Mh.mgeni rasmi katika mashindano hayo,Mh Samuel Lazaro akisalimiana na wachezaji wa timu zote mbili
mawaidha yamekolea wakati wa hafutaimu.

Friday, November 20, 2009

OMBEA TANZANIA

We must pray jamani, kuna wenzetu wanaishi katika mazingira magumu sana. angalia picha then utakubaliana nami kuwa tanzania tumebarikiwa na tunatakiwa kuiombea











Thursday, November 19, 2009

JUST BE YOURSELF

hiyo parking yake nimeipenda

Sasa jamani hiyo nyumba ina umeme kweli? maana jamaa ana dish vp kuna hata viti vya kukalia wageni? lakini jamaa kaamua kuwa kipeke yake peke yake bwana