Thursday, September 30, 2010

MAPOKEZI YA WANAMUZIKI WA FEREE GOLA WALIPOTUA DAR JANA

. Mwimbaji na rapa mahiri wa mwanamuziki Ferre Gola kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo anayejulikana kama (Shikito) akipewa escot na Baunsa mara baada ya kuwasili usiku wa kuamkia leo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K,Nyerere.(Kwa Wahusika naomba nidhamu ya Baunsa huyu ambaye kwa bahati mbaya sikuweza kulibaini jina lake mapema,naomba ichunguzwe kwa makini awapo kazini) .! Mwimbaji na rapa wa Mwanamuziki Ferre Gola kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo anayejulikana kama (Shikitu) akihojiwa na wanahabari kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K,Nyerere, hata hivyo Kiongozi wao mwanamuziki Ferre Gola anatarajiwa kuwasili leo mnamo saa 12 jioni na anatarajia kufanya onyesho kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kesho Ijumaa akishirikiana na bendi ya Mashujaa inayoongozwa na Mwanamuziki Jado Field Force. Mmiliki wa bendi ya Mashujaa ajulikanae kwa jina la Mama Sakina,akiwaomba radhi baadhi ya waandishi wa habari usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa kimataifa wa Mwl JK Nyerere,Kufuatia kutukanwa kwao na baadhi ya Mabaunsa waliofika uwanjani hapo huku wakiwa wamelewa,Mama Sakina pia alitoa ufafanuzi wa vurugu zilizotokea uwanjani hapo wakati wa kumpokea Ferre Gola,akieleza kuwa watu hao walikuwa wametumwa kwa ajili ya kuja kumuharibia mapokezi hayo wakiwemo na baadhi ya Mabaunsa ambao walikuwa wamelewa kupita kiasi huku wakitukana matusi mazito mazito kwa Waandishi wa habari waliokuja uwanjani hapo kufanya kazi yao. Mwanamuziki mpiga gitaa la Sollo kutoka kundi la Ferre Gola anayejulikana kama Chally Sollo akihojiwa na vyombo vya habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K. Nyerere mara baada ya kuwasili kwa ajili ya onyesho lao linalotarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kesho Ijumaa. Baadhi ya Wanamuziki wa Bendi ya Mashujaa wakiongozwa na kiongozi wa bendi hiyo Jado Field Force (haonekani pichani) katika kutia nakshi nakshi ujio wa mwanamuziki Ferre Gola (Shetani) wakati walipokuwa wakimsubiri mwanamuziki huyo kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K.Nrerere usiku wa kuamkia leo, pamoja na shamra shamra hizo Mwanamuziki huyo hakuweza kuwasili usiku wa jana,badala yale anatua leo jioni jijini Dar mnamo majira ya saa 12 na ushehe hivi,waliotangulia ni wanamuziki wake.

No comments:

Post a Comment