Thursday, September 30, 2010

DR. GHALIB BILAL ALIPOKUWA MKOANI MBEYA

Mgombea Mwenza wa Urasi wa Tanzania kupitia CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Ileje, Aliko Kibona, wakati alipofika katika jimbo hilo jana Sept 29 kufanya mkutano wa kampeni katika kujiandaa na uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31 nchini kote. (Picha na Muhidin Sufiani)
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal na mkewe Zakia Bilal, wakiinua mikono kuwasalimia wananchi wa Kijiji cha Ilembo Wilaya ya Mbeya Vijijini, wakati walipowasili kijijini hapo juzi Sept 28 kufanya mkutano wa kampeni.
Wananchi wa Kijiji cha Ilembo Wilaya ya Mbeya Vijijini, wakicheza ngoma ya asili ya kabila la Wanyakyusa, wakati wa mapokezi ya mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk Mohamed Gharib Bilal, alipofika katika Kijiji hicho juzi Sept 28 kufanya mkutano wa kampeni.
Wananchi wa Kijiji cha Ilembo Wilaya ya Mbeya Vijijini, wakimsikiliza Mgombea mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji hicho juzi Sept 28.

No comments:

Post a Comment