Wednesday, September 29, 2010

MISS TANZANIA 2010 AKABIDHIWA BENDERA TAYARI KUELEKEA CHINA

Mshindi wa taji la ulimbwende nchini Tanzania kwa mwaka 2010(Miss Tanzania 2010),Genevieve Emmanuel, asubuhi ya leo hii(kwa saa za Tanzania) amekabidhiwa rasmi bendera ya Tanzania tayari kabisa kwenda kuiwakilisha nchi katika mashindano ya ulimbwende ya dunia(Miss World 2010) yanayotarajiwa kufanyika huko Sanya nchini China tarehe 30 Oktoba 2010.Anatarajiwa kuondoka nchini kesho.

Shughuli ya kumkabidhi bendera mrembo huyo ilifanyikia katika viwanja vya Tanzania Investment Centre(TIC) jijini Dar-es-salaam na kuhudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa kituo hicho cha uwekezaji,Bw.Emmanuel Ole Naiko, Miss Tanzania 2009,Miriam Gerald, Mratibu wa Miss Tanzania,Hasheem Lundenga,wawakilishi wa wadhamini wa shindano la Miss Tanzania kutoka kampuni ya mawasiliano,Vodacom na wengineo.

Miss Tanzania 2010,Genevieve Emmanuel(kushoto) na Miss Tanzania 2009,Miriam Gerald.

Mashindano ya mwaka huu yanaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo.Awali mashindano ya mwaka huu yalikuwa yafanyikie nchini Vietnam lakini nchi hiyo ilijiondoa katika uandaaji huo na hivyo China kupewa nafasi ya kuyaandaa

No comments:

Post a Comment